Gavana Tutuba afungua kikao maboresho ya utoaji mikopo kwa wananchi na urejeshaji kidijitali

DAR-Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Bw. Emmanuel Tutuba amefungua kikao kazi kilichoandaliwa na Wakala wa Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Zanzibar (ZEEA) kwa kushirikiana na Kampuni ya Airpay Tanzania chenye lengo la kuboresha utoaji wa mikopo kwa wananchi na urejeshaji kidijitali.
Gavana Tutuba amesema urejeshaji huo wa mikopo kwa urahisi utatumia mfumo wa malipo uliotengenezwa na Airpay Tanzania ambao utaweza kutunza data na kubaini mlipaji mzuri na mbaya kwa hatua zaidi.
Aidha, Gavana Tutuba ametoa wito kwa vikundi pamoja na watu wote wanaokopa fedha serikalini na kwenye mabenki kutumia fedha hizo vizuri na kuzirejesha kwa wakati ili wengine waweze kukopa pia.
Washiriki wengine wa mkutano huo ni pamoja na mabenki, kampuni zinazotoa huduma ya mawasiliano ya simu za Tanzania Bara na Zanzibar. pamoja na Kampuni za kuchakata taarifa za mikopo (Credit Reference Bureau.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news