ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dkt.Hussein Ali Mwinyi amewashukuru wasanii wote kwa kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuwaletea maendeleo wananchi, tangu ameingia madarakani wamekuwa wakijitolea kufikisha ujumbe kupitia sanaa ya burudani na kuitangaza Zanzibar.


Naye Ali Saleh Kiba amemuahidi Rais Dkt.Mwinyi kujitolea bega kwa bega kutangaza mafanikio ya Zanzibar kupitia sanaa yake ya muziki na kituo chake cha habari cha Crown Media kuwapa habari wananchi kwa ujumla.