Watoto walioibwa na mganga kwa kushirikiana na dada wa kazi wapatikana

DAR-Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limefanikiwa kuwapata watoto wawili Husna Gulam (3) na Mahdi Mohamed (4) walioibiwa na dada wa kazi kwa kushirikiana na mganga wa kienyeji nyumbani kwao Tandika jijini Dar es Salaam.
Kamanda wa Kanda Maalum Dar es Salaam, Jumanne Muliro amesema watoto hao wamepatikana Januari 14, 2025 nyumbani kwa mganga huyo Abdulkarim Shariff (43), Kimara Baruti jijini Dar es Salaam, ambapo walipelekwa Hospitali kwa ajili ya kufanyiwa vipimo na hawajakutwa na tatizo lolote.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news