DODOMA-Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla amewasilisha muhtasari wa mafanikio ya utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kipindi cha 2020-2025.
Mheshimiwa Abdulla ameeleza hatua kubwa zilizopigwa katika sekta mbalimbali zikiwemo uchumi na elimu kote Unguja na Pemba.
Hayo ameyabainisha leo Januari 19, 2025, wakati wa Mkutano Mkuu Maalumu wa CCM katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete jijini Dodoma.

Pia, Pato la Taifa limepanda kutoka shilingi trilioni 4.2 mwaka 2020 hadi trilioni 6.288 mwaka 2024, jambo linaloashiria maendeleo makubwa katika ustawi wa taifa.

Pia amesema,Serikali imefanikiwa kujenga shule mpya 116 zenye jumla ya madarasa 2,713, ikiwemo shule 35 za ghorofa.

Mheshimiwa Abdulla amesema, ufaulu wa wanafunzi wa kidato cha nne umeongezeka kutoka asilimia 55.4 mwaka 2020 hadi asilimia 85.6 mwaka 2023, huku ufaulu wa kidato cha sita ukifikia asilimia 99.9 mwaka 2024. Tazama video kwa kina zaidi hapa;