DAR-Kiungo mshambuliaji wa Yanga, Stephane Aziz Ki amemuoa rasmi mwanamitindo Hamisa Mobetto katika hafla ya ndoa iliyofanyika leo, Februari 16, 2025 katika Msikiti wa Masjid Nnuur, Mbweni jijini Dar es Salaam.
Ndoa hiyo imefungwa na Sheikh Mkuu wa Dar es Salaam, Walid Alhad Omar akisaidiana na jopo la masheikh wengine.


Februari 15,2025 Aziz Ki alilipa mahari ya ng’ombe 30 na shilingi milioni 30, mahari iliyokabidhiwa kwa familia ya bibi harusi na Rais wa Yanga, Mhandisi Heris Said kwa niaba ya bwana harusi.