Bidhaa za vyakula zitakuwepo za kutosha wakati wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani-Rais Dkt.Mwinyi

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt.Hussein Ali Mwinyi amesema,Serikali imefanya juhudi maalum za kuhakikisha bidhaa za vyakula zinakuwepo za kutosha wakati wa Ramadhani.
Alhaj Dkt. Mwinyi amesema hayo alipozungumza katika Kongamano la Kumi la Kuukaribisha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani Ukumbi wa Idrissa Abdulwakil Kikwajuni.

Amesema kuwa, Serikali imeandaa mazingira wezeshi ya uingizaji wa bidhaa hizo hapa nchini.
Halikadhalika, Dkt.Mwinyi ameendelea kuwahimiza wafanyabiashara kutopandisha bei za bidhaa wakati wa Ramadhani pamoja na kufuata bei elekezi ili kuwapa unafuu wananchi kumudu kununua.

Akizungumzia suala la amani wakati nchi ikielekea katika Uchaguzi Mkuu mwaka huu amewasisitiza wanasiasa,viongozi wa dini na waandishi wa habari kupaza sauti zao kuhubiri amani ili nchi iendelee kuwa na utulivu.
Alhaj Dkt.Mwinyi ameipongeza Jumuiya ya Zanzibar Welcoming Ramadhan Conference kwa kuandaa kongamano hilo kwa mafanikio kwa miaka kumi mfululizo na kuridhia ombi la kulifanya kuwa la Kimataifa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news