LINDI- Basi lililobeba wachezaji wa timu ya mpira wa miguu ya Dodoma Jiji limepinduka na kutumbukia mtoni katika eneo la Nangurukuru mkoani Lindi likiwa na wachezaji.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi9URrbRxMKVF3ZXQt_VEw_N5-JbtAMzjEEGRxnh7k3ant-vGSTbM7ZnUsrrKAoyQO8pP-caL7RXbk6snDZm-BvsRR6pY4IHe5S_lAV2VyvGJy-qbo6QjtDYFIRzGVTH0ElDBi2MfUpg1luN2rokADL_zBITPu0aJFYJKJAH5Irn_V32nlmpsRL1v7zeNWJ/s16000/1001185506.jpg)
Katibu Mkuu wa timu hiyo, Fortunatus Johnson amethibitisha tukio hilo akieleza kuwa wachezaji wote wamejeruhiwa kwa kukatwa na vioo vya gari.
Dodoma Jiji FC kupitia mchezo huo uliopigwa Uwanja wa Majaliwa uliopo Ruangwa dhidi ya wenyeji Namungo FC waliambulia sare ya mabao 2-2.