Imetosha! Wananchi wa Bumbuli wamkataa January Makamba

TANGA-"Kwa miaka 15 sasa, wananchi wa Jimbo la Bumbuli tumekuwa tukihadaiwa na ahadi zisizotekelezeka. Tumeshuhudia mbunge wa msimu, anayejitokeza tu nyakati za uchaguzi kama mtalii, kisha kutoweka bila kutatua matatizo yetu ya msingi. Leo, kwa umoja wetu, tunasema January Makamba IMETOSHA!.
"Jimbo letu limebaki nyuma kimaendeleo, huku wananchi wakikosa huduma muhimu kama maji safi, barabara za uhakika, huduma bora za afya, na fursa za kiuchumi. 

"Tumechoka na tunasema hatutamchagua tena January Makamba. Tunamtaka apumzike, na tunatoa wito kwa Chama cha Mapinduzi (CCM) kutusikiliza, kwani sauti ya wananchi ni sauti ya Mungu.
"Wananchi wa kata zote 18 za Jimbo la Bumbuli kwa kauli moja tunasema:

1. Baga

2. Bumbuli

3. Dule "B"

4. Funta

5. Kisiwani

6. Kwemkomole

7. Mahezangulu

8. Mamba

9. Mayo

10. Mbuzii

11. Mgwashi

12. Milingano

13. Mponde

14. Nkongoi

15. Soni

16. Tamota

17. Usambara

18. Vuga

"Tumesema kwa kauli moja, January Makamba hatufai tena! CCM isituangushe kwa kupuuza sauti yetu. Yeyote atakayepuuza ujumbe huu ataanguka ANGUKO KUU."

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news