Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi Kuu ya NBC yatoa maamuzi kwa klabu, faini mbalimbali

DAR-Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi imefuta adhabu ya kadi nyekundu kwa mchezaji wa Namungo, Derick Mukombozi, aliyoadhibiwa na mwamuzi wa mchezo wa Namungo FC dhidi ya Simba SC.
Kamati imefikia uamuzi huo baada ya kujiridhisha kuwa maelezo yaliyopo kwenye ripoti ya mwamuzi hayana ushahidi wa kutosha unaoendana na marejeo ya picha mjongeo.

Aidha, mchezaji wa Namungo, Daniel Amoah ameadhibiwa kwa kutozwa faini ya shilingi 500,000, kwa kosa la kuonekana akimwaga vimiminika kwenye goli, jambo lililohusianishwa na vitendo vinavyoashiria imani za kishirikina.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news