DODOMA-Kamati ya Ukaguzi ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imeshiriki katika Mafunzo maalumu yanayohusiana na masuala mbalimbali ya Ukaguzi, yanayoendeshwa na wakufunzi kutoka Wizara ya Fedha, Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Ndani wa Serikali.

Mafunzo hayo yanafanyika kwa siku mbili (2) kuanzia tarehe 20 hadi 21 Februari, 2025 katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ulioko Mtumba, Jijini Dodoma.