Magazeti leo Februari 1,2025

JAMHURI ya Kidemokrasi ya Congo imetoa wito Rwanda iwekewe vikwazo na kupunguzwa kwa misaada na pia isimamishwe ushiriki wake katika misheni ya kulinda amani ya UN kwa jukumu ambalo inadaiwa kutekeleza katika mzozo wa Congo Mashariki.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Congo DR, Therese Kayikwamba aliiambia BBC, Rwanda inakalia eneo la nchi yake kinyume cha sheria.

Therese amesema Rwanda inaunga mkono, kufadhili na kuandaa ujasusi ambao unatafuta kupindua serikali iliyochaguliwa kisheria.
Wakijibu suala hilo, Msemaji wa Serikali ya Rwanda Yolande Makolo amesema nchi yake inatetea mipaka yake wala haina nia ya mabadiliko ya serikali.

Viongozi wa waasi ambao walichukua udhibiti wa baadhi ya sehemu za Jiji la Goma wiki hii walisema Alhamisi kwamba wanakusudia kufika Kinshasa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news