Mama Mariam Mwinyi aendelea na ziara yake nchini Sharjah

SHARJAH-Mke wa Rais wa Zanzibar, Msarifu na Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini ya Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF), Mhe.Mama Mariam Mwinyi ameendelea na ziara yake nchini Sharjah kwa kutembelea Kituo cha Ulinzi wa Watoto cha Kanaf.
Aidha, Mama Mariam Mwinyi amefahamishwa kuhusu huduma za kituo hicho ikiwa ni pamoja na msaada wa haraka wa kisheria, kisaikolojia na jamii kwa waathirika wa unyanyasaji wa watoto.

Vilevile Mama Mariam Mwinyi ametembelea Baraza la Sanaa la Kisasa la IRTH (ICCC) mpango unaolenga kuhifadhi urithi na utamaduni wa Emarati kwa kuunganisha ufundi wa jadi na ubunifu wa kisasa.
Mama Mariam Mwinyi amepongeza mpango huo kama mfano mzuri wa uwezeshaji, urithi na ufundi.

Pia ametembelea Sharjah Children, Shirika Tanzu la RubiQam Foundation for Creating Leaders and Innovators.

Kituo hicho kina jukumu la kukuza maendeleo ya ujuzi,kuimarisha utambulisho wa Taifa na maadili ya pamoja.
Halikadhalika Mama Mariam Mwinyi amesifu Juhudi za Sharjah za kuwawezesha na kuwajumuisha Watoto katika Maisha ya Umma.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news