Mama Mariam Mwinyi awasili Ethiopia

ADDIS ABABA-Mke wa Rais wa Zanzibar, Msarifu na Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini ya Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF) Mama Mariam Mwinyi ameondoka Zanzibar na kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Bole, Addis Ababa Nchini Ethiopia leo Februari 14, 2025.
Katika Uwanja wa Kimataifa nchini humo alipokelewa na Viongozi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Ethiopia na Mkuu wa Itifaki, Wizara ya Mambo ya Nje Ethiopia Balozi, Dkt. Aziza Gelete.
Mama Mariam Mwinyi ataungana na Wake wa Marais wengine kutoka nchi wanachama wa Taasisi ya Maendeleo ya Wake wa Marais wa Afrika (OAFLAD) katika Mkutano wa 29 wa Kawaida wa Mwaka. Mkutano huu unalenga kwa kiasi kikubwa kupambania haki za uongozi kwa wanawake.
Mkutano huu unafanyika kando ya Mkutano wa Kawaida wa 38 wa Wakuu wa Serikali Wanawake wa Umoja wa Afrika (AU).

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news