Mapokezi ya Rais Dkt.Mwinyi yatikisha Pemba, wanachama 2,439 wa ACT wajiunga CCM

ZANZIBAR-Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar,Dkt.Hussein Ali Mwinyi amezisisitiza jumuiya za Chama Cha Mapinduzi kuwahamasisha wanachama na wananchi kujiandikisha na kujitokeza kwa wingi kupiga kura ili CCM ishinde kwa kishindo.
Dkt. Mwinyi ambaye ni Mgombea Mteule wa Urais wa Zanzibar kwa Tiketi ya CCM ameyasema hayo alipozungumza na Wanachama na Wananchi Mauwani, Kiwani Mkoa wa Kusini Pemba Katika Mkutano Maalum wa Mapokezi yake baada ya Kuteuliwa hivi Karibuni kuwa Mgombea wa Urais wa Zanzibar.

Dkt.Mwinyi amesema kumekuwa na tabia ya baadhi ya Wana CCM kutojitokeza kupiga kura wakati wa Uchaguzi jambo linaloipunguzia Kura za Ushindi Chama hicho.
Aidha, Rais Dkt. Mwinyi ameipongeza UWT kwa kazi nzuri walioifanya ya uhamasishaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga kura na kuiagiza kuendelea na mwamko huo.

Halikadhalika Dkt.Mwinyi amewapongeza na kuwakaribisha wanachama 2,439 wa Chama cha ACT Wazalendo kwa uamuzi wa kujiunga na CCM kwani wamefanya uamuzi sahihi na kuwaahidi ushirikiano wa kiwango cha juu.

Amempongeza Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi,Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuiendesha nchi kwa mafanikio na kudumisha amani.
Mapema asubuhi wanachama wa Chama Cha Mapinduzi walijitokeza kumpokea Dkt. Mwinyi alipowasili Uwanja wa Ndege wa Pemba wakiongozwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Hemed Suleimani Abdalla.

Hatimaye alizungumza na wazee wa CCM Afisi ndogo ya Chama Cha Mapinduzi Chakechake na baadae msafara huo ukaelekea katika Mkutano na Wanachama Mauwani Kiwani ambapo wana CCM walijipanga barabarani kumlaki Dkt. Mwinyi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news