Mawaziri Dkt.Nchemba na Profesa Mkumbo wafanya mazungumzo na Ujumbe kutoka Benki ya Dunia

DODOMA-Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb) na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo, wamekutana na kufanya mazungumzo na Ujumbe kutoka Benki ya Dunia ukiongozwa na Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia, anayeziwakilisha pia nchi za Malawi, Zambia na Zimbabwe, Bw. Nathan Belete, katika Ofisi za Wizara ya Fedha (Treasury Square), jijini Dodoma, ambapo pamoja na mambo mengine wamejadiliana namna ya kuongeza ushirikiano katika kuendeleza biashara na uwekezaji kwa kushirikiana na Sekta Binafsi.
Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bi. Amina Khamis Shaaban, Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, Dkt. Mursali Milanzi, Naibu Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango, anayeshughulikia Utendaji na Tathmini, Dkt. Linda Ezekiel na Viongozi wengine waandamizi wa Wizara ya Fedha, Tume ya Mipango na Maafisa wengine waandamizi kutoka serikalini.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news