MV Kilindoni chasimama kutoa huduma kupisha matengenezo

PWANI-Kivuko cha Mv Kilindoni kinachotoa huduma kati ya Mafia wilayani Mafia na Nyamisati wilayani Kibiti mkoani Pwani kitasimama kutoa huduma katika eneo hilo kuanzia Februari 12, 2025 ili kupisha matengenezo pamoja na kufungwa injini mpya.
Kivuko cha Mv Kilindoni kiliwasili kikiwa na abiria pamoja na mizigo eneo la Nyamisati kikitokea eilayani Mafia.

Kivuko hicho kinapelekwa mkoani Dar es Salaam ambako kitakuwa huko kwa muda wa wiki moja kikifanyiwa matengenezo hayo ili kukiongezea ufanisi kiweze kurejea kikiwa bora na salama kwa watumiaji.

Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) umewaomba radhi abiria wote kutokana na usumbufu watakaoupata kutokana na kukosekana kwa huduma ya kivuko hicho.

International news

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post