Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika awasili Tanzania

DAR-Balozi wa Tanzania katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Mhe. Said Mshana amempokea Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Mhe. Moussa Faki Mahamat aliyewasili nchini Tanzania alfajiri ya Februari 8, 2025 kuuwakilisha Umoja wa Afrika katika Mkutano wa Dharura wa Pamoja Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) utakaofanyika hapo baadaye.

Jumuiya zote mbili zinakutana kujadili kwa lengo la kupatia ufumbuzi hali ya ulinzi na usalama katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news