Ninawakaribisha wananchi wote katika uzinduzi wa Kampeni ya Sisi ni Wamoja-Mama Mariam Mwinyi

ZANZIBAR-Mke wa Rais wa Zanzibar, Msarifu na Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini ya Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation, Mama Mariam Mwinyi anawakaribisha Wananchi wote katika uzinduzi wa Kampeni ya Sisi ni Wamoja #WeAreEqual inayosimamiwa na Taasisi ya Wake wa Marais wa Afrika(OAFLAD)
Kampeni hii itazinduliwa kesho tarehe 28/02/2024, saa 12 asubuhi katika viwanja vya Hospitali ya Kitogani, Mkoa wa Kusini Unguja katika kilele cha kambi ya Matibabu na upasuaji wa bure ya "Afya Bora, Maisha Bora" inayoendelea viwanjani hapo.

Wake wa Marais watashiriki akiwemo Mke wa Rais wa Burundi Mama Angeline Ndayubaha Ndayishimiye, Mke wa Rais wa Kenya Mama Rachel Ruto, wawakilishi kutoka Nigeria,Angola na Afisa Mtendaji Mkuu wa OAFLAD.

Aidha ,Tanzania itakuwa nchi ya 22 kati ya 54 kuzindua kampeni hii chini ya uwakilishi wa Mhe.Mama Mariam Mwinyi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news