Rais Dkt.Mwinyi amjulia hali Mwanazuoni Sheikh Ali Hemed Jabir Alfarsy

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dkt.Hussein Ali Mwinyi amemjulia hali Mwanazuoni Maarufu Sheikh Ali Hemed Jabir Alfarsy (Maalim Aliyan)nyumbani kwake Mchangani Wilaya ya Mjini ,Mkoa wa Mjini Magharibi.
Sheikh Aliyan ambaye ni Imamu Mkuu wa Masjid Maghfirah wa Mchangani pia aliwahi kuwa Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA),hivi karibuni alilazwa katika Hospital ya Aga Khan jijini Dar es Salaam alipokuwa akitibiwa na hatimaye kurejea Zanzibar na hali yake inaendelea vizuri.
Rais Dkt.Mwinyi amekuwa na utaratibu endelevu wa kuwatembelea wananchi mbalimbali hususani wagonjwa na kuwafariji pamoja na kuwaombea dua njema.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news