Rais Dkt.Mwinyi amuapisha Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA)

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dkt.Hussein Ali Mwinyi amemuapisha Kamishna Mkuu Mpya wa Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA),Said Kiondo Athumani aliyemteuwa hivi karibuni.
Hafla hiyo imefanyika leo Ikulu jijini Zanzibar na kuhudhuriwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar,Hemed Suleiman Abdulla,viongozi mbalimbali wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar,watendaji wakuu wa taasisi za umma na wakuu wa vikosi vya ulinzi na usalama.
Kabla ya uteuzi huo, Kamishna Kiondo alikuwa Mkufunzi Mkuu wa Chuo cha Kodi cha Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news