Rais Dkt.Samia abariki uwekezaji shamba la miwa Pangani

TANGA-Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, amebariki uwekezaji mkubwa wa Wizara ya Kilimo wa shamba la miwa Wilayani Pangani mkoani Tanga.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Kumba Wilayani Pangani akiwa katika muendelezo wa ziara yake ya siku nane mkoani Tanga Rais Dkt Samia, amesema uwekezaji huo katika sekta ya kilimo utafungua fursa ya ajira na uchumi kwa mkoa huo.

Amesema, Serikali inakwenda kuwekeza katika kilimo kikubwa cha miwa katika bonde la Pangani na kujenga viwanda vingi vya sukari ili kujitosheleza na bidhaa hiyo.
"Viwanda vingi vya sukari vilivyopo nchini vinazalisha sukari ya kawaida ya kula kuna sukari ya viwandani ambayo inaagizwa kwa wingi kutoka nje, sasa hili kuhifadhi na ku ‘save’fedha za kigeni tumeamua kikwanda hiki kijengwe ndani ya Tanga na kitajengwa Pangani, hatua hii ni kufungua fursa zaidi na kutengeneza ajira za wananchi,”amesema

“Barabara hii pia itakwenda kuchochea kwa wingi kilimo cha mihogo, nazi na kilimo kingine maeneo hayo na wakulima kuuza bidhaa zao nje ya Tanga,”amesema.
Mapema Mbunge wa Pangani ambaye ni Waziri wa Maji,Juma Aweso, amesema wamekuwa na mazungumza mazuri na Waziri wa Kilimo Hussein Bashe ya kutumia maji ya mto Pangani kufanya uwekezaji wa Kilimo kikubwa cha mashamba ya miwa hatua ambayo itasaidia vijana wengi kupata ajira.

“Tumezungumza na kaka yangu Waziri Bashe na ameahidi kufanya uwekezaji wa kilimo kikubwa cha miwa na vijana wetu kuweza kupata ajira,”amesema Aweso.
Aweso amesema, hatua hiyo inayotokana na ujenzi wa barabara ya Pangani ambayo inakwenda kufungua fursa ya uwekezaji mkubwa kiuchumi katika sekta ya kilimo cha miwa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news