Rais Dkt.Samia ateua viongozi sita leo Februari 13,2025

ZANZIBAR-Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali na kumpangia kituo cha kazi Balozi.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka, uteuzi na kupangiwa kituo ni kama ifuatavyo:

Dkt. Amina Suleiman Msengwa ameteuliwa kuwa Mtakwimu Mkuu wa Serikali. Kabla ya uteuzi huu, Dkt. Msengwa alikuwa Mhadhiri Mwandamizi Chuo Kikuucha Dar es Salaam.

Dkt. Msengwa anachukua nafasi ya Dkt. Albina Chuwa ambaye amemaliza muda wake;

Jaji Dkt. Ntemi Nimilwa Kilekamajenga ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Masoko na Mitaji.

Jaji Dkt. Kilekamajenga anachukua nafasi ya Jaji Dkt. Deo John Nangela ambaye aliteuliwa kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani;

Prof.Aurelia Kamuzora ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi yaBodi ya Kahawa. Prof. Kamuzora ameteuliwa kwa kipindi cha pili;

Bw. Abdulmajid Nsekela ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenziwa Bodi ya Chai Tanzania.

Bw. Nsekela anachukua nafasi ya Bw. Mustafa HamisUmande ambaye amemaliza muda wake;

Prof. Hozen Kahesi Mayaya ameteuliwa kuwa Mkuu wa Chuo cha Mipango yaMaendeleo Vijijini (IRDP). Prof. Hozen ameteuliwa kwa kipindi cha pili; na

Balozi Dkt. Habib Galuss Kambanga amepangiwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Rwanda.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news