Rais Dkt.Samia ateua wawili, Balozi Kaganda apelekwa Zimbabwe

TANGA-Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa viongozi na kumpangia kituo cha kazi Balozi.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Februari 27,2025 na Katibu Mkuu Kiongozi,Balozi Dkt.Moses Kusiluka, uteuzi na kupangiwa kituo ni kama ifuatavyo:

-(i) Dkt.Fred Matola Msemwa ameteuliwa kuwa Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango.

Kabla ya uteuzi huu, Dkt. Msemwa alikuwa Afisa Mtendaji Mkuu wa Watumishi Housing Investments (WHI);

(ii) Prof. Philipo Lonati Sanga ameteuliwa kuwa Mkuu wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW).

Kabla ya uteuzi huu, Prof. Sanga alikuwa Mhadhiri Mwandamizi katika Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima.

Prof.Sanga anachukua nafasi ya Prof.Michael Ngumbi ambaye amemaliza muda wake;na

(iii) Balozi Susan Salome Kaganda amepangiwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo,uapisho wa Katibu Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Mipango utafanyika kwa tarehe itakayopangwa baadaye.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news