Rais Dkt.Samia azindua tume mbili kwenda Ngorongoro

DAR-Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluahu Hassan amezindua Tume ya Rais ya Kutathmini kuhusu Masuala ya Mgogoro wa Ardhi katika Eneo la Hifadhiya Ngorongoro na Tume ya Rais ya Kutathmini Zoezi la Uhamaji wa Hiari wa Wakazi wa Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro.
Uzinduzi wa tume hizo mbili umefanyika Ikulu Magogoni jijini Dar es Salaam ikiwa ni utekelezaji wa ahadi iliyotolewa na Rais Dkt. Samia tarehe 01 Disemba 2024 mkoani Arusha alipokukutana na kuzungumza na viongozi na wawakilishi wa wananchi wanaoshi eneo la Ngorongoro na maeneo jirani.
Tume hizo mbili zitaongozwa na Mhe. Jaji Dkt. Gerald Ndika ambaye ni Mwenyekiti wa Tume ya Kutathmini kuhusu Masuala ya Mgogoro wa Ardhi katika Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro na Mhandisi Musa Iyombe ambaye ni Mwenyekiti wa Tume ya Kutathmini Zoezi la Uhamaji wa Hiari wa Wakazi wa Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro.
Aidha, tume hizo mbili zinajumuisha uwakilishi wa wananchi wanaoishi katika eneo la Ngorongoro na zinatarajia kufanya kazi kwa kipindi cha miezi mitatu.
Pamoja na mambo mengine, wakati wa uzinduzi wa Tume hizo mbili, Rais Dkt Samia ameeleza imani yake kuwa kazi itakayofanywa na Tume hizo itawezesha kupatikana kwa suluhu ya kudumu ya changamoto zilizowasilishwa kwake na viongozi na wawakilishi wa wananchi wanaoishi kwenye eneo la Ngorongoro.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news