Serikali yasisitiza ushirikiano kwa Masheha

ZANZIBAR-Katibu Mtendaji wa Baraza la Vijana Zanzibar, Ali Haji Hassan amewataka Masheha kuwa na ushirikiano katika kuhakikisha wanayaimarisha mabaraza ya vijana katika Shehia wanazoziongoza.
Akizungumza na Masheha kutoka Shehia za Wilaya ya Mjini na Wilaya ya Magharibi B, amesema Masheha wana jukumu la kuhakikisha kuwa vijana wanajiunga na Baraza la Vijana Zanzibar na kufanya hivyo ni kuisadia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya kufikia lengo kuanzishwa kwa Baraza la Vijana.

Amesema, Masheha si viongozi tu wa wananchi bali ni walezi wa vijana hivyo kutumia busara na hekima zao kuhakikisha vijana wanajiunga na kuwa na wanachama wa Baraza la Vijana Zanzibar ili kupata fursa zitolewazo na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na taasisi binafsi kupitia Baraza la Vijana Zanzibar.
"Kujiunga na Baraza la Vijana Zanzibar kwa kijana kuna faida na fursa azipatazo kijana akiwa mwanachama ikiwa ni pamoja na kupatiwa mafunzo yatakayowawezesha kujiajiri na Kuajirika,"alisema Katibu huyo.

Aidha,amewaomba Masheha hao kushirikiana na Baraza la Vijana Zanzibar kutafuta njia sahihi ya kutatua changamoto za Vijana ikiwa ni pamoja na kujiingiza katika matumizi ya dawa za kulevya na vitendo vya udhalilishaji.
Kwa upande wa Mjumbe wa Baraza la Watendaji wa Baraza la Vijana Zanzibar Farid Mohammed Haji amewataka Masheha kuwahamasisha Vijana walio na sifa za kujiandikisha kujitokeza kwa wingi Kujiandikisha katika Daftari la kudumu la Wapiga kura ili kushiriki Uchaguzi Mkuu kwa kuchagua viongozi watakaoliongoza Taifa.

Akizungumza Sheha wa Shehia ya Mchina,Bi. Zam Zam Ali Rijali ameiomba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuwapatia Vijana kuwapatia Miradi itakayowawezesha kujikwamua Kimaisha kupitia Shehia zao.
Aidha, Sheha wa Shehia ya Muembe Ladu Khamis Omar ameliomba Baraza la Vijana Zanzibar kushuka chini kwenye ngazi ya Shehia kufanya hivyo kutasaidia kuyaimarisha mabaraza ya Vijana kwa ngazi hiyo.

Baraza la Vijana Zanzibar kupitia Kikao hicho limeadhimia kuandaa utaratibu wa Kuzungumza na Masheha kila baada ya miezi mitatu kwa lengo la kupeana mrejesho na kuyaimarisha mabaraza.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news