Serikali yatoa angalizo kwa asasi za kiraia Zanzibar

ZANZIBAR-Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ,Mhe. Masoud Ali Mohammed, amesema Serikali, haitopenda kuona asasi za kiraia kubadilisha muelekeo na kujiingiza katika mambo yasiokuwa na faida kwa taifa.
Akizungumza na viongozi wa asasi za kiraia huko Tunguu, amesema serikali imekuwa ikizihitaji asasi hizo katika kuimarisha huduma za kijamii na maendeleo, hivyo sio vyema kuona zinakiuka malengo ya kuanzishwa kwake.
Amezihakikishia asasi hizo kuwa Serikali itaendelea kuzilinda kwa kuzipa muongozo ili kuziepusha kujiingiza katika migogoro isiyo ya lazima ambayo haina faida kwa wananchi na taifa lao.

Naye Mrajis wa Jumuiya zisizo za kiserikali Zanzibar NGO'S, Ahmed Khalid Abdallah, amesema uwasilishaji wa taarifa za fedha na utendaji kazi wa Jumuiya hizo kwa kila mwaka ni jambo la kisheria.

Amesema, kuwasilishwa kwa taarifa hizo kunaiwezesha ofisi ya mrajis kuandika ripoti na kuiwasilisha Serikalini ili kutambulika jinsi ya utendaji kazi wa jumuiya hizo.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa Kusini Unguja Ayoub Mohamed Mahmoud, amesema Mkoa huo unaendelea kufunguka kiuchumi na ustawi wa jamii kupitia mchango wa asasi za kiraia, ikiwemo ujenzi wa kituo cha afya Kizimkazi na ujenzi wa kituo cha kusaidia wajasiriamali Wilaya ya Kati.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news