Simba SC nguvu moja kwa Fountain Gate FC

MANYARA-Kocha Msaidizi wa Simba Sports Club, Darian Wilken amesema maandalizi ya mchezo wa leowa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Fountain Gate FC utakaopigwa Uwanja wa Tanzanite Kwaraa yamekamilika.
Wilken amesema, mchezo utakuwa mgumu hasa kutokana na Fountain Gate kuwa nyumbani, lakini wamejiandaa vizuri kuhakikisha wanapata pointi tatu muhimu ugenini.

Wilken ameongeza kuwa, mzunguko wa pili wa ligi ni mgumu na kila timu imejipanga kuhakikisha inafanya vizuri hasa ikiwa nyumbani,lakini wamejiandaa kupambana na changamoto yoyote itakayojitokeza.

“Maandalizi yamekamilika, kikosi kimefika leo Manyara na jioni kitafanya mazoezi ya mwisho kwa ajili ya mchezo wa kesho ambao tunaamini utakuwa mgumu,” amesema Wilken.

Kwa upande wake nahodha wa timu Mohamed Hussein ‘Zimbwe Jr’ amesema, kwa upande wao wachezaji wapo tayari kupambana hadi mwisho kuhakikisha alama tatu zinapatikana.

“Malengo yetu kwenye kila mchezo ni kuhakikisha tunapata alama tatu, kwetu kila mechi ni fainali na tupo tayari kupambana hadi mwisho ili kufanikisha hilo,” amesema Zimbwe Jr.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news