Simba SC yatozwa faini

DAR-Klabu ya soka ya Simba SC, imetozwa faini ya shilingi milioni moja kwa kosa la walinzi wake kuwazuia walinzi wa uwanjani (stewards) kumkamata shabiki aliyekuwa akitaka kuingia uwanjani baada ya mchezo wao dhidi ya Singida Black Stars uliopigwa Desemba 28, 2024.

Kwa mujibu wa taarifa ya Kamati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) pia imeeleza Kocha wa Fountain Gate FC, Robert Matano ametozwa faini ya shilingi laki tano kwa kosa la kuwashutumu waamuzi waliochezesha mechi yao dhidi ya Simba SC iliyopigwa Februari 6, 2025.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news