Chuo cha SUA waanza kuuza mbegu bora za malisho ya mifugo

MOROGORO-Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo kimeanza kuuza mbegu bora za malisho ya mifugo ambapo kupitia Kitengo cha Nyanda za Malisho kimewakaribisha wafugaji kuchangamkia fursa hiyo.
Bw. Winfred Ngilangwa kutoka Idara ya Shamba la Mafunzo SUA ameeleza hayo Februari 6, 2025 wakati wakivuna mbegu za malisho zilizonunuliwa na Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela ya mkoani Arusha ambapo ametumia nafasi hiyo kuwakaribisha wafugaji binafsi kufika chuoni kununua hizo mbegu.

Bw. Ngilangwa amesema mpaka sasa SUA imeuza kilo 8000 ambazo ni sawa na tani 8 za nyasi aina ya Juncao ambazo hutumia miezi mitatu kukua tangia kupandwa kwake.
"Katika shamba hili la mafunzo hapa SUA tuna zaidi ya aina 10 ya nyasi ambazo zinaweza kupandwa katika maeneo tofauti tofauti nchini, wafugaji tunawakaribisha kununua nyasi hizi pia tunatoa ushauri wa kitaaluma,"alisema.

Kwa upande wake, Bw. Yeremia Ntandu akizungumzia mwitikio wa wafugaji kununua mbegu za nyasi amesema kumekuwa na mwitikio mzuri ambapo wafugaji wamekuwa wakinunua kila mmoja kwa mahitaji yake huku akibainisha kuwa ukuzaji wa hizo nyasi ni rahisi kwani hauna gharama kubwa.
Idara ya Shamba la Mafunzo imejikita katika kuzalisha nyasi za malisho za aina mbalimbali zinazotumika kutengeneza chakula kwa mifugo pamoja na mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi wanaosomea Shahada zinazoendana na shughuli hizo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news