TAKUKURU Njombe yafuatilia miradi yenye thamani ya shilingi bilioni 15.8

NJOMBE-Kaimu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Njombe Noel Mseo, alihabarisha umma kupitia vyombo vya habari na kueleza kuwa katika Mkoa wa Njombe wamefuatilia utekelezaji wa miradi ya maendeleo 32 ya thamani ya shilingi bilioni 15.8 katika kipindi cha Oktoba hadi Desemba, 2024.
Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TAKUKURU Njombe Februari 7,2025 ambapo kati yake, miradi tisa yenye thamani ya shilingi Bilioni 13.1 ilionekana kuwa na kasoro ndogondogo na ushauri ukatolewa ili kurekebisha kasoro hizo.

Mkuu huyo alieleza kuwa, katika kuhakikisha ubora wa miradi hiyo, Kamati za Ujenzi zinazosimamia utekelezaji wa miradi zilipewa elimu ya namna ya kutekeleza miradi hiyo na kudhibiti ubadharifù unaoweza kutokea katika utekelezaji wa miradi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news