Tanzania na Hungary zasaini Hati ya Makubaliano katika eneo la mafunzo ya Kidiplomasia

BUDAPEST-Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Hungary zimesaini Hati ya Makubaliano (MoU) ya Ushirikiano katika eneo la Mafunzo ya Kidiplomasia.
MoU hiyo inalenga kubadilishana ujuzi na uzoefu pamoja na kubadilishana wanafunzi wa diplomasia ili kupata elimu itakayokidhi uhitaji wa sasa ambapo wadau wakuu ni Kituo cha Uhusiano wa Kimataifa cha Dkt. Salim Ahmed Salim kwa upande wa Tanzania na Chuo cha Diplomasia cha Hungary.
Hati hiyo imesainiwa jijini Budapest, Hungary na Waziri wake Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Tanzania, Mhe. Mahmoud Thabit Kombo (Mb.), pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara wa Hungary, Mhe. Péter Szijjártó.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news