VIDEO:MAMBO 12 YA MIEZI 12 YA BADRU PSSSF KWENYE UZINDUZI WA PAPERLESS BARAZA MEETING LEO


Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya PSSSF, Bi. Joyce Mapunjo (wa tatu kushoto), akitoa cheti cha utambuzi wa huduma bora kwa Bw. Abdallah Adam wa PSSSF (wa kwanza kulia), kutokana na wateja kuridhika na jinsi anavyo wahudumia. Mwingine aliyepewa tuzo hiyo ni Bi. Amina Kassim (hayupo pichani), Meneja wa PSSSF Kanda ya Ilala jijini Dar es Salaam. Wa pili kulia ni Bw. Abdul-Razaq Badru, Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la PSSSF na wa kwanza kulia ni Katibu wa Baraza hilo, Steve BIKO.

Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Bw. Abdul-Razaq BADRU, akiongea na Waandishi wa Habari baada ya uzinduzi wa Mfumo wa Vikao vya Baraza hilo, pasipo kutumia Karatasi (PSSSF paperless Baraza Meeting Proceedings) katika hoteli Regency & Resort, kandokando mwa Ziwa Singidani, katika Manispaa ya Singida, leo Februari 6, 2025). Sambamba na hilo, Bw. Badru leo ametimiza miezi 12 ya utumishi katika Mfuko wa PSSSF na ameainisha mambo 12 kuelezea uongozi wake katika taasisi hiyo. Bw. Badru ametoa shukran nyingi kwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyemteua, Wizara - Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Ajira, Vijana, na Wenye Ulemavu), Bodi ya Wadhamini, Menejimenti na Wafanyakazi wote wa Mfuko huo.
Mfumo wa kutotumia karatasi katika nyaraka za vikao, utakaosaidia kupunguza gharama, muda wa kuandaa makabrasha, na kusaidia kuongeza ufanisi zaidi, umezinduliwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa PSSSF, Bi. Joyce Mapunjo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news