Wasira amjulia hali Gachuma

MWANZA-Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Stephen Wasira amemjulia hali Mjumbe wa Halmashauri Kuu yaTaifa (NEC), ndugu Christopher Gachuma ambaye amelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda, Bugando jijini Mwanza.
Ndugu Gachuma amelazwa hospitalini hapo baada ya kupata ajali ya gari katika Kijiji cha Gesarya, Kata ya Lung'abure, wilayani Serengeti Mkoa wa Mara alipokuwa akielekea katika Ziara ya Makamu Mwenyekiti Wasira.

Majeruhi mwengine katika ajali hiyo ni Mkuu wa Wilaya ya Serengeti, ndugu Kemilembe Ruta pamoja na dereva wa gari hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa ya hospitali hiyo, majeruhi wote wa ajali hiyo wanaendelea vizuri.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news