Waziri Kabudi akutana na viongozi wa Chama cha Wachapishaji wa Vitabu Tanzania (PATA)

DODOMA-Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi amekutana na viongozi wa Chama cha Wachapishaji wa Vitabu Tanzania (PATA) katika ofisi zake jijini Dodoma kwa ajili ya kuangalia fursa maridhawa katika kubadilishana uzoefu na kuimarisha sekta ya uandishi na uchapishaji wa vitabu Tanzania.
Katika kikao hicho Waziri Kabudi amewasisitiza chama hicho kutafsiri vitabu vilivyo katika lugha nyingine kuja katika Kiswahili fasaha na sanifu.

Pia, amewahamasisha kuchapisha vitabu vya hadithi fupifupi ambavyo vitapata soko katika nchi mbalimbali zinazoridhia ufundishwaji na ujifunzwaji wa Kiswahili.
Aidha, ameahidi kuwa Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) litatumia majukwaa mbalimbali ya ndani na nje ya nchi kunadi vitabu hivyo kwa kuwa sekta ya Uandishi na Uchapishaji wa vitabu ni muhimu katika kuhifadhi, kueneza na kuendeleza maarifa na kurithisha historia na utambulisho wa utamaduni wetu.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news