Waziri Mchengerwa akutana na wanaotaka kuifanya Dar kama Abu Dhabi

DODOMA-Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa amekutana na wawakilishi wa Kampuni ya Straling Holding ya Abu Dhabi na kujadili namna bora ya ujenzi wa mji mpya wa kisasa katika Jiji la Dar es Salaam.
Waziri Mchengerwa amekutana na Kampuni ya Straling Holding leo Februari 14,2025 kwenye ukumbi TAMISEMI jijini Dodoma ambao wameonesha nia ya kuwekeza kwenye ujenzi wa miundombinu ya barabara, madaraja, elimu, afya, bandari, umeme wa maji, reli, mifumo ya umwagiliaji, madini na viwanda nchini.
Mhe. Mchengerwa amefanya kikao kazi na wawekezaji hao ili kuwa na uelewa wa pamoja juu ya shughuli wanazozifanya, ili kuona kama kuna haja ya kushirikiana nao katika ujenzi wa mji mpya wa kisasa katika jiji la Dar es Salaam kwa kuzingatia maslahi mapana ya taifa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news