DAR-Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Februari 17, 2025 amemwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye kilele cha maadhimisho ya miaka 20 ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu, inayofanyika kwenye Kituo cha Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam.
Maadhimisho hayo yaliambatana na kliniki za huduma katika mikoa 7 nchini yakilenga kutoa elimu kwa wadau muhimu wa masuala ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu.