Waziri Mkuu ashiriki maziko ya Bi.Asina Omari

LINDI-Waziri Mkuu na Mbunge wa Jimbo ya Ruangwa Mheshimiwa Kassim Majaliwa leo Februari 22, 2025 ameshiriki katika mazishi ya marehemu Bi. Asina Omary Nyimbilile mkazi wa Kata ya Nkowe, Ruangwa mkoani Lindi.
Akizungumza na waombolezaji katika mazishi hayo, Mheshimiwa Majaliwa amewataka ndugu, jamaa na marafiki kumuombea marehemu Bi. Asina pumziko la milele pamoja na kuyaenzi yote mema aliyofanya wakati wa uhai wake.
Bi. Asina amezikwa katika makaburi ya jumuiya yaliyopo katika kata ya Nkowe.

Maziko hayo pia yamehudhuriwa na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Lindi Ndugu Hassan Jarufu, Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, Hassan Ngoma na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Ruangwa Ndugu Ibrahim Ndoro.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news