Wizara yaandaa Tamasha la Biashara la Eid El Fitri

ZANZIBAR-Katika kuadhimisha Sikukuu ya Eid El Fitri, Wizara ya Biashara na Maendeleo ya Viwanda imeandaa Tamasha la Biashara la Eid El Fitri kwa ajili ya wajasiriamali hivyo tunaombwa kuchangamkia fursa ya kushiriki kwenye tamasha hilo litakalofanyika kuanzia tarehe 30 Machi hadi 4 Aprili 2025, katika viwanja vya maonesho Dimani, Zanzibar.

Tamasha hili linatarajiwa kuwa jukwaa muhimu la kukuza biashara, kuonyesha bidhaa na huduma mpya, na kuvutia wateja kutoka maeneo mbalimbali.

Lengo kuu ni kutoa nafasi kwa wajasiriamali
kuonyesha ubunifu wao, kuimarisha uhusiano wa kibiashara, na kufungua milango ya fursa za
kibiashara kwa wageni na wakazi wa Zanzibar.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news