DAR-Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imeendelea kusherehekea Siku ya Wanawake Duniani kwa kufanya shughuli mbalimbali za kijamii zinazoakisi mshikamano na mchango wa wanawake katika maendeleo ya taifa.


Katika hotuba yake, Bi. Msemo aliwasihi wanawake kuwa mabalozi wa haki, usawa, na uwezeshaji katika kila nyanja ya maisha. Alisisitiza umuhimu wa kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia misingi ya maadili, utu, na hekima.
Moja ya shughuli muhimu zilizofanywa na wanawake wa BoT ni kuchangia fedha kwa ajili ya kusaidia wahitaji, ambapo walifanikiwa kununua viti vya magurudumu 24.
Aidha, walichangia kiasi cha fedha kwa Taasisi ya Ali Kimara Rare Disease Foundation, ambayo inahudumia watoto wanaoishi na magonjwa adimu.