BoT yaendesha semina kwa Kamati ya Bunge kuhusu utekelezaji wa Sera ya Kupunguza Matumizi ya Fedha Taslimu

DODOMA-Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imeendesha semina kwa Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Utekelezaji wa Sera ya Kupunguza Matumizi ya Fedha Taslimu.
Semina hiyo imefanyika katika ofisi za Bunge jijini Dodoma tarehe 28 Machi 2025.

Ujumbe wa Benki Kuu katika semina hiyo uliongozwa na Mkurugenzi wa Benki Kuu wa Mifumo ya Malipo ya Taifa, Bi. Lucy Shaidi na wasilisho kufanywa na Meneja Msaidizi, Bw. Mushumbusi Mutashobya. 

Wengine katika ujumbe huo walikuwa ni Meneja Msaidizi kutoka Kurugenzi hiyo upande wa leseni na sera, Bw. Fabian Kasole.
Katika semina hiyo, waheshimiwa wajumbe wa kamati chini ya mwenyekiti wao, Mhe. Oran Njeza (Mbeya Vijijini) walihimiza kuchukuliwa kwa hatua zaidi ili kukuza matumizi ya fedha kidijitali na kuchochea ukuaji wa uchumi. Aidha, walitoa wito wa kupunguzwa kwa gharama zinazotozwa kila wakati mtu anapofanya miamala ya fedha kidijitali.
Wametaka wadau wote katika sekta ya fedha kushirikiana kuongeza matumizi ya fedha za kidijitali, pamoja na kupunguza gharama za matumizi hayo ya fedha katika kufanya malipo kwa huduma na bidhaa. 

Ujumbe wa Wizara ya Fedha katika semina hiyo uliongozwa na Kamishna Msaidizi, Bi. Dionisia Mjema.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news