Cuba yaguzwa na mageuzi makubwa ya kiuchumi Zanzibar, Rais Dkt.Mwinyi asisitiza ushirikiano

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dkt.Hussein Ali Mwinyi amesema, Zanzibar ina kila sababu ya kuimarisha ushirikiano na Cuba kutokana na mchango unaotolewa na nchi hiyo kwa maendeleo ya Zanzibar.
Rais Dkt. Mwinyi amesema hayo alipozungumza na Rais wa Baraza la Taifa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Cuba, Esteban Lazo Hernandez na Ujumbe wake waliofika Ikulu Zanzibar.
Aidha,Rais Dkt.Mwinyi ameishukuru Cuba kwa misaada inayoendelea kuitoa kwa Zanzibar, kwani imekua ikichangia kwa kiasi kikubwa maendeleo katika sekta tofauti hususan Sekta ya Afya na kuimarisha ustawi wa wananchi wa Zanzibar.

Halikadhalika Rais Dkt.Mwinyi amesema,ujio wa ujumbe huo ni fursa muhimu ya kufungua maeneo mengine ya ushirikiano ikiwemo Uchumi wa Buluu, Elimu, Utalii, Teknolojia,Utamaduni na Michezo.
Naye Rais wa Baraza la Taifa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Cuba, Esteban Lazo Hernandez ameihakikishia Zanzibar kuendelea na ushirikiano na kupongeza mabadiliko makubwa yaliofikiwa na Zanzibar katika ujenzi wa viwanja vya ndege,miundonbinu ya barabara,hospitali na vituo vya afya hapa nchini.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news