Dkt.Mpango ashiriki Maombolezo ya Kitaifa na Ibada ya kumuaga Baba wa Taifa la Namibia hayati Dkt.Sam Nujoma

WINDHOEK-Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Maombolezo ya Kitaifa na Ibada ya kumuaga aliyekuwa Rais na Baba wa Taifa la Namibia hayati Dkt. Sam Nujoma iliyofanyika katika Uwanja wa Michezo wa Uhuru uliopo jijini Windhoek nchini Namibia.
Maombolezo ya Kitaifa na Ibada ya kumuaga hayati Dkt. Nujoma yamehudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Bara la Afrika na Mataifa mbalimbali nje ya bara la Afrika.
Hayati Dkt. Sam Nujoma alifariki tarehe 08 Februari 2025 na Mazishi ya kiongozi huyo yanatarajiwa kufanyika tarehe 01 Machi 2025 katika Makaburi ya Mashujaa Jijini Windhoek nchini Namibia.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news