DAR-Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba (Mb), ameshiriki uzinduzi wa huduma za kidigitali za Benki ya NBC (NBC Kiganjani App) inayomwezesha mteja kupata huduma za kibenki kigigitali kwa kutumia simu za mkononi tukio ambalo, Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa alikuwa Mgeni Rasmi, lililofanyika katika Ukumbi wa The Super Dome, Masaki jijini Dar es Salaam.

Aidha, Mhe. Dkt. Nchemba, aliipongeza Benki hiyo kwa kudhamini Ligi Kuu ya Tanzania Bara (NBCPL) ambayo kupitia udhamini wao imekuwa na msisimko mkubwa na kuiwezesha Tanzania kupanda viwango na kuwa ligi namba 4 kwa Ubora baranı Afrika.