GSM Foundation wamepata milioni 925, Tone Tone sijui wamepata ngapi?

DAR-Ninakumbuka, viongozi walipokuwa Gerezani tulifanya fundraising siku tatu tukapata pesa.
Hao viongozi wa chama wakiongozwa na Tundu Lissu wajiulize leo mbona hawapati wachangiaji? Badala yake wanajaza walinzi ukumbini tu.

Wanaishia kutudhalilisha tu, kwamba Makao Makuu watu wanalipwa kidogo sana, wakati wa kampeni walisema uongo mkubwa sana kwamba tulilipwa mamilioni.

Kuna aina fulani ya maumivu naipata,ila watavuna walichopanda muda ni dawa sahihi sana sana.

Ni jambo la kushangaza GSM Foundation ndani ya saa chache wamepata zaidi ya shilingi milioni 925, lakini Tone Tone pengine kwa siku kadhaa hawajafikisha hata shilingi milioni 100.

Hii, inadhirisha kuwa, kuna mahali kama chama tumekwama na wananchi wengi wametuchoka. Tujitafakari.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news