Iran na Tanzania kuendeleza ushirikiano


Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El maamry Mwamba (wapili kushoto), akiongoza kikao, katika ukumbi wake wa mikutano, jijini Dodoma, alipotembelewa na kufanya mazungumzo na Balozi wa Iran nchini Tanzania, Mhe. Dkt. Mohammed Nikhal (wapili kulia), kikao ambacho pia kimewahusisha Wataalam wa Wizara ya Fedha, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) pamoja na wataalam kutoka, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El maamry Mwamba, akizungumza katika kikao na Balozi wa Iran nchini Tanzania, Mhe. Dkt. Mohammed Nikhal, (hayupo pichani), alipotembelea Ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.
Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El maamry Mwamba akiteta jambo na Kamishna wa Idara ya Usimamizi wa Deni la Serikali, Wizara ya Fedha, Bw. Japhet Jastine, katika kikao kati yake na Balozi wa Iran nchini Tanzania, Mhe. Dkt. Mohammed Nikhal, (hayupo pichani), Treasury Square, jijini Dodoma.
Balozi wa Iran nchini Tanzania, Mhe. Dkt. Mohammed Nikhal, akizungumza, katika kikao kati yake na Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El maary Mwamba, Treasury Square, jijini Dodoma.
Baadhi ya wataalam wa Wizara ya Fedha, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) pamoja na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, wakifuatilia kwa karibu kikao kati ya Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El maamry Mwamba na Balozi wa Iran nchini Tanzania, Mhe. Dkt. Mohammed Nikhal, jijini Dodoma.
Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El maamry Mwamba na Balozi wa Iran nchini Tanzania, Mhe. Dkt. Mohammed Nikhal, wakiwa katika picha na ya pamoja Timu ya Wataalamu wa Wizara ya Fedha, Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki pamoja na Ubalozi wa Irani Tanzania, baada ya kumaliza kikao maalum, katika Ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.
Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El maamry Mwamba na Balozi wa Iran nchini Tanzania, Mhe. Dkt. Mohammed Nikhal, wakiwa katika picha na ya pamoja, baada ya kumaliza kikao maalum, katika Ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Fedha - Dodoma).

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news