Mzee Moris Nyunyusa kujengewa Mnara jengo jipya la TBC

DODOMA-Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma amesema kuwa jengo jipya la Makao Makuu ya TBC Dodoma litasheheni mambo mengi ikiwemo makumbusho ya utamaduni ambapo mzee Moris Nyunyusa na ngoma zake 10 ni miongoni mwa vivutio kwenye jengo hilo.
Mhe. Mwinjuma ameyasema hayo Jumatano, Machi 12, 2025 wakati alipotembelea jengo hilo linalojengwa Vikonje, jijini Dodoma na kamati ya kudumu ya Bunge ya Habari, elimu, Utamaduni na Michezo iliyoongozwa na Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Husna Sekiboko.

Hayati mzee Nyunyusa ni mlemavu wa macho ambaye alivuma kwa umahiri wake wa kupiga ngoma 17 ambapo moja ya mdundo wake ulitumiwa na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) na redio Tanzania kuashiria kuanza kwa taarifa ya habari.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news