Ofisi ya Rais-UTUMISHI katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani 2025

NA VERONICA MWAFISI

OFISI ya Rais-UTUMISHI katika kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani 2025 inatoa huduma za Kiutumishi katika Viwanja vya Sheikh Amri Abeid Karume kuanzia tarehe 01 hadi 8 Machi, 2025 jijini Arusha.
Watumishi wa Umma na Wananchi wote wanakaribishwa kutembelea Banda la Ofisi hiyo kwa ajili ya kupata huduma mbalimbali za kiutumishi.

Huduma zinazotolewa katika Banda hilo ni Mifumo ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Serikalini ikiwemo e-Watumishi (HCMIS), e-Msawazo (HR-Assessment), e-Uhamisho (Watumishi Portal), e-Mikopo, e-Utendaji, e-Likizo pamoja na e-Mrejesho.
Vilevile katika banda hilo zinapatikana Huduma za Kisheria katika Utumishi wa Umma na hitimisho la kazi kwa kwa Mtumishi wa Umma pamoja na Huduma za Ujumuishwaji wa Anuai za Jamii Mahali Pa Kazi katika Utumishi wa Umma.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news