Omolo asisitiza uandaaji wa Mpango wa Bajeti wenye tija

DODOMA-Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Bi. Jenifa Christian Omolo, amewasisitiza Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakurugenzi wa Halmashauri pamoja na Maafisa Bajeti wa Mikoa kuandaa Mpango wa Bajeti wa Mwaka 2025/2026 wenye tija.
Ametoa msisitizo huo jijini Dodoma, wakati akihitimisha kikaokazi cha siku mbili cha Uchambuzi wa Bajeti na Mipango kwa Mwaka 2025/26.
Kikao hicho kiliwaleta pamoja wadau wa sekta husika ili kuainisha na kuibua maeneo ambayo mafungu yanaweza kushirikiana na kuleta ufanisi katika uandaaji na utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Mwaka 2025/26.
Uchambuzi huo unalenga kuhakikisha uratibu wa shughuli za Serikali Kisekta unaboreshwa ili kuongeza ushirikiano na nguvu ya pamoja (Synergies) katika utekelezaji wa mipango kati ya Sekta zinazotegemeana.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news