Pamba Jiji FC wapata ajali

DODOMA-Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imetuma salamu za pole kwa klabu ya Pamba Jiji FC kufuatia ajali ya basi lao iliyotokea Bahi mkoani Dodoma leo saa 11:00 alfajiri.
Wachezaji wa timu hiyo walikuwa safarini kutoka Bukoba mkoani Kagera kuelekea Morogoro kwa ajili ya mchezo wa Kombe la Shirikisho la Benki ya CRDB, Machi 11, 2025 dhidi ya Kiluvya United.

"Tunawatakia nafuu ya mapema wote waliopata maumivu na Mungu awasimamie katika safari yao. Amin!."

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news