Rais Dkt.Mwinyi afuturisha wananchi Mkoa wa Kaskazini Pemba,asisitiza upendo na mshikamano

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt.Hussein Ali Mwinyi amejumuika na wananchi katika makundi maalum wakiwemo Wazee, Yatima, Watu wenye Ulemavu, Wajane, Walimu wa Madrasa, Masheikh, na Maimamu wa Misikiti wa Mkoa wa Kaskazini Pemba katika Futari ya pamoja aliyoiandaa.
Hafla hiyo imefanyika Baraza la Wawakilishi, Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba tarehe 19 Machi 2025.
Aidha, Rais Dkt.Mwinyi amewasisitiza wananchi kuendelea kuiombea nchi amani wakati huu ikielekea katika Uchaguzi Mkuu pamoja na viongozi wakuu wa nchi.

Wakati huo huo, Rais Dkt. Mwinyi amekabidhi Sadaka ya Futari kwa Watu wa Makundi Maalum wa Mkoa wa Kaskazini Pemba wakiwemo Wajane, Yatima, Watu wenye Ulemavu, Wazee,Walimu wa Madrasa na Maimamu wa Misikiti.
Rais Dkt.Mwinyi amehitimisha zoezi hilo mkoa wa mwisho leo kwa Mikoa yote ya Unguja na Pemba kwa kujumuika pamoja na Wananchi katika futari na kuwakabidhi sadaka makundi maalum wenye uhitaji.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news